Sunday, July 6, 2014

UMOJA WA WANAWAKE LUDEWA{UWALU} WATOA MISAADA KATIKA HOSPITALI YA LUDEWA



mganga mkuu wa wilaya Bwana Msengi katikati akipoke misaada hiyo


UWALU wakionesha baadhi ya vifaa hivyo



Bwana msengi akizungumza jambo na wanawake wa UWALU

Umoja wa wanawake ludewa [UWALU] waishio dare es salaam Umetoa misaada mbali mbali ya vifaaa katika hospitali ya wilayani hapa ukilenga zaidi huduma ya akina mama na watoto.
amesema hayo hii leo katibu wa chama hicho B, Sarah wakati akisoma risala fupi mbele ya mganga mkuu wa wilaya Bw.Msengi Mwendo ambapo amesema chama hicho kilianzishwa na akina mama hao kwa lengo la kushiriki katika shughuli za kijamii,kama vile kuchangia
katika huduma za afya,elimu pamoja na maafa.
Akikabidhi vifaa mbele ya mganga mkuu wa wilaya ludewa B, Sarah amesema kuwa umoja huo umetoa vifaa kama vifaa kama vile Vitanda vya kuzalishia,vitanda vya kujifungulia,mashuka90, blanketi 50 pamoja na troli ya kubebea dawa.
Aidha kwa upande wa mganga mkuu wa hospitali hoyo Bw.Msengi ameushukuru umoja wa aikina mama hao kwani wamegusa nyanja ambazo mara nyingi kumekuwa na na changamoto nyingi katika utoaji huduma hususani kwa aikana mama wajawazito pamoja na watoto wadogo ukizingatia ludewa sasa imekuwa na ongezeko kubwa la watu kutoka sehemu mbalimbali.


Pia bw, Msengi Ameiomba jamii kwa ujumla kuanzisha vikundi mbali mbali kwani vimekuwa ni msaada mkubwa katika kuchangia na kuchochea huduma bora za kijamii.

No comments:

Post a Comment